Ngoja leo niongee na wale akinadada ambao wamejiwekea vigezo na masharti mengi sana katika aina ya mwanaume wanayemtaka. Sikatai
kwamba lazima kuna vigezo vyamsingi vichache ambavyo kila mwanamke ni
muhimu kuvizingatia na kuviheshimu lasivyo utaolewa na mwanaume tu na
sio mume. Lakini wapo sasa wale wenye masharti milioni nzima, ukisikia
wakivitaja vigezo vyao kuhusu mume wanayemtaka utadhani wanakwenda
kuolewa mbinguni. Masharti utadhani mtu anaingia mkataba na benki kumbe
ni ishu ya mume tu. Hivi unataka kuolewa na malaika au na mtu? Na kama
ni mtu basi na wewe ni mtu na sio malaika, mtu huoa au kuolewa na mtu na
sio vinginevyo. Dont be overambitious ukajipalilia mazingira ya stress
zisizo lazima. Wewe jione bado binti wakati ishara za sura hadi tabia
zinaonyesha kuwa mshale unakaribia kusoma uzee. Mwisho ukijakuhamaki na
kupunguza masharti unaambulia kibabu. Kuwa makini na smart pia -

No comments:
Post a Comment