Thursday, May 7, 2015

Kama Bado Hujajiunga Nami, Unaweza Kujiunga Hapa Nikutumie Habari Moja Kwa Moja




Idadi kubwa ya wanawake wanaofanya biashara ya ngono Mjini Kahama wamedaiwa kugoma kutumia dawa ya kupunguza makali ya virusi vya ukimwi licha ya kupima na kubainika wanaishi na maambukizi ya ugonjwa huo badala yake hutumia kula nyama ya kitimoto kwa madai inapunguza kasi hiyo kuliko dawa za ARV.

Hali hiyo imeelezwa jana Mjini Kahama na afisa maendeleo ya jamii Mjini Kahama Fanuel Ruben ambaye amesema ofisi yake imefanya ukaguzi kwenye madanguro yanayotumiwa na wanawake hao kwa biashara ya ngono na kubaini wapo wasichana kati ya miaka 15 hadi 20.

Ruben amesema baada ya kubaini hiyo wamewachukua wasichana na kuwafanyia vipimo wengi wao wamebainika kuwa na ujauzito na maambukuzi ya virusi vya ukimwi hali iliyoonyesha wanafanya ngono bila kutumia kinga ya maambukizi ya magonjwa ya kuambukiza.


Hata hivyo amesema wasichana hao baada ya kuwafanyia uchunguzi wamegoma kutumia dawa za kupunguza makali kwa madai wenzao wanaoishi na virusi vya ukimwi hutumia nyama ya kitimoto badala ya dawa hiyo.

Kufuatia hali hiyo Ruben amesema ameandaa mkakati wa kuwachukulia hatua wale wote wanaofanya biashara ya ngono huku wakijua wao ni waathirika wa ugonjwa huo kwa kuwa ipo sheria mpya inayokataza mwathirika wa virusi vya ukimwi kuwaambukiza wenzake kwa makusudi.

Kauli hiyo imekuja baada ya mkuu wa Wilaya ya Kahama Benson Mpesya kutangaza msako wa kuyafunga madanguro yote yanayotumiwa na wanawake hao kwa biashara ya ngono baada ya kubainika wengi wa wateja wao ni vijana wadogo ambao wanahatarisha maisha yao.
SOURCE FARAJA BLOG

No comments:

BREAKING NEWS; MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2018 HAPA

 BFYA LINK HAPA CHINI KUYAPATA>>>>> http://41.59.85.98/results/2018/acsee/acseex.htm

Logo

Logo Design by FlamingText.com